Posts

Showing posts from January, 2017

SOMA MAGAZETI YA LEO MWISHO WA MWEZI JANUARY,HABARI KUU WAGENI WANAOINGIA MAREKANI WAPEKULIWA FACEBOOK

Image

MAALIM SEIF AFUNGUKA MAZITO KUHUSIANA NA UONGOZI WA ZANZIBAR

Image
Aliyekuwa  mgombea urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amesema yupo tayari kufanya tena maridhiano endapo pande zote mbili zitakubali kwamba Zanzibar kuna matatizo. Maalim Seif aliyasema hayo jana katika kipindi cha Funguka kinachorushwa na Televisheni ya AZAM na kuongozwa na mtangazaji nguli nchini, Tido Mhando. Alisema maridhiano yaliyofanyika akiwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Dk. Amani Abeid Karume,  yalikuwa na manufaa makubwa kwa kuwa Zanzibar ilikuwa na amani na utulivu. Maalim Seif alisema CUF iliamua kukaa na Karume baada ya kuona uchaguzi ulikuwa unakaribia kufanyika hivyo ikaamua kufanya kikao cha muafaka wa maridhiano na kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK) iliyozaa matunda. Alisema baada ya kufanyika maridhiano na kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais alikuwa na nafasi kubwa ya kumshauri Rais mambo mbalimbali.  “Hata kulipokuwa na SUK (Serikali ya Umoja wa Kitaifa),  mambo yalikuwa mazuri na maelewano na hata

NJIA YA RELI KATI YA DAR ES SALAAM NA RUVU YAFUNGULIWA

Image
Uongozi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) umetoa taarifa kuwa kuanzia saa 9 alasiri leo Januari 30, 2017 njia ya reli kati ya Kituo Kikuu cha Dar es salaam na Ruvu imefunguliwa rasmi kwa shughuli za uendeshaji wa reli. Taarifa hiyo imesema kuwa kazi ya ufunguaji njia imewezekana baada ya Wahandisi na Mafundi wa reli kuyaondoa Mabehewa yaliopata ajali  kutoka relini na pia kuikarabati sehemu iliyoharibika . Kazi hiyo imefanyika kuanzia usiku wa Januari 29, 2017 hadi mchana wa Januari 30, 2017. Aidha treni ya abiria iliyoahirisha safari ya kuondoka kwenda bara jana imeondoka leo saa 9:05 alasiri kutoka kituo kikuu cha Dar es Salaam kwenda bara.. Wakati huo huo imefahamika kuwa msafiri mmoja aliyetambulikana kama Nd Basekena O. Bango kutoka Bujumbura Burundi akiwa anasafiri kutoka Kigoma amelazwa katika Hospitali ya Tumbi Kibaha mkoani wa Pwani kwa ajili ya matibabu zaidi. Aligunduliwa kuwa amechanika mguu wake wa kulia hivyo basi kuhitaji kushonwa mguu wake huo. Taarif

MKUTANO WA 6 WA BUNGE KUENDELEA DODOMA MAPEMA HII LEO

Image
Mkuu wa Kitengo cha Habari, Elimu na Masiliano Ofisi ya Bunge, Owen Mwandumbya akizungumza na wanahabi mjini Dodoma leo akitoa taarifa ya yale yatakayojiri katika Mkutano wa sita wa Bunge la 11 unaotaraji kuanza leo Januari 31 hadi Februari 10 mwaka huu mjini Dodoma. *************** Mkutano wa Sita wa Bunge unatarajiwa kuanza siku ya Jumanne tarehe 31 Januari 2017 na kumalizika tarehe 10 Februari 2017 Mjini Dodoma.  Mkutano huo utakuwa ni mahususi kwa ajili ya kupokea Taarifa za mwaka za Kamati za Kudumu za Bunge ambapo Kamati 14 za kisekta na mtambuka zitawasilisha taarifa zake Bungeni katika kipindi hiki. Shughuli nyingine zitakazofanyika katika Mkutano huu ni kama ifuatavyo:-   1.0           KIAPO CHA UAMINIFU Kufuatia uteuzi wa wabunge watatu walioteuliwa na Mhe. Rais Dk. John Pombe Magufuli hivi karibuni na Uchaguzi Mdogo uliofanyika katika Jimbo la Dimani, Zanzibar Tarehe 22 Januari 2017, kutakuwa na Kiapo cha Uaminifu kwa Wabunge wapya wanne ambao ni:- (i)      

MHUBIRI ALIYEKUWA NA WAKE 86 AFARIKI NIGERIA

Image
Haki miliki ya picha Image caption Mohammed Bello Abubakar huenda alikuwa na zaidi ya wake 100 Mhubiri mmoja wa zamani wa Kiislamu nchini Nigeria ambaye alikuwa na takriban wanawake 86 ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 93. Mohammed Bello Abubakar alifariki nyumbani kwake katika jimbo la Niger siku ya Jumamosi, kutokana na ugonjwa ambao haukutajwa Watu wengi walihudhuria mazishi yake siku ya Jumapili. Gazeti la Nigeria la Daily Trust liliripoti kuwa alipokuwa na wake 86 mwaka 2008 wakati aliangaziwa na vyombo vya habari, idadi hiyo ilipanda hadi wake 130 wakati wa kifo chake. Mzee mwenye watoto 70 na wajukuu 300 Tanzania Wengine wao walikuwa wajawazito. BBC iliripoti mwaka 2008 kuwa alikuwa na takriban watoto 170 lakini gazeti hilo lilisema kuwa aliwaacha watoto 203.

MWENYEKITI WA CCM ANUSURIKA KUPIGWA RISASI MBEYA

Image
Mwenyekiti wa CCM Mbeya Mjini, Efrahim Mwaitenda mwenye umri wa miaka 60 amejeruhiwa kwa kupigwa risasi mgongoni na mtu au watu wasiofahamika.   Mwenyekiti wa CCM Mbeya Mjini (Aliyekaa) akipelekwa hospitali) Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Emmanuel Lukula amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe 29.01.2017 majira ya saa 05:45 usiku katika kitongoji cha Ilopa, Kijiji cha Mahenge, Kata ya Makwale, Tarafa ya Ntebela, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya. Amesema tukio hilo limetokea wakati akiwa amelala kitandani nyumbani kwake Ntembela ambapo mbinu iliyotumika ilikuwa ni  kukata wavu wa dirisha na kumjeruhi kwa kutumia silaha za kienyeji zinazotumia risasi za gololi. Mwenyekiti huyo amefikishwa Hospitali ya Rufaa ya Mbeya na hali yake inaendelea vizuri. Lukula amewaambia waandishi wa habari kuwa nia ya shambulizi hilo ilikuwa ni kutaka kuumua na kwamba juhudi za kuwatafuta na kuwakamata wahusika zinaendelea

MOROCO YAKUBALIWA KUJIUNGA UPYA NA AU

Image
Mfalme Mohammed VI, ambaye alishiriki kikao cha Umoja wa Afrika Jumatatu wiki hii mjini Addis Ababa, alifanya ziara nyingi za kikazi katika miji mikuu ya nchi za Afrika ili kupata uungwaji mkono. REUTERS/Maghreb Agence Press/Pool Viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wamemua Jumatatu wiki  hii kuikubalia Morocco kujiunga upya na Umoja wa Afrika. Wakati huo huo Tume ya Umoja wa Afrika imempata kiongozi mpya, huku rais wa Guinea, Alpha Condé, alkichaguliwa kuwa rais wa Umoja wa Afrika Angalau Marais na viongozi wa serikali 39 kati ya 54 wanachama wa Umoja wa afrika wamepiga kura ya ndio kwa Morocco kujiunga upya na AU, kwa mujibu wa rais wa Senegal Macky Sall, ambaye ameshiriki katika zoezi la kuchunguza faili ya Morocco Jumatatu wiki hii mjini Addis Ababa, nchini Ethiopia. Rais wa Liberia Ellen Johnson Sirleaf, amethibitisha kuwa "nchi nyingi wanachama wa Umoja wa Afrika walibaliwa ombi la Morocco kurejea katika Umoja wa Afrika." Mwaka 1984, Morocco

ZAIDI YA WATU MILIONI MOJA WASAINI BARUA KUMZUIA TRUMP KUZURU UINGEREZA

Image
Haki miliki ya picha PA Image caption Waziri Mkuu Teresa May alitangaza muwaliko huo wakati akiwa ziarani Marekani. Zaidi ya watu milioni moja wa Uingereza wamesaini barua ya kutoa shinikizo kwa serikali ya Uingereza kusitisha ziara rasmi iliopangwa baadaye mwaka huu ya rais Donald Trump. Barua hiyo iliyoandikwa kufuatia agizo la rais Trump dhidi ya wahamiaji, inaeleza kuwa kuja kwake kutamuaibisha Malkia Elizabeth. Idadi ya watu wanaoendelea kusaini kupinga Mwaliko wa Trump nchini Uingereza inaendelea kuongezeka, tangu Marekani kuweka vikwazo dhidi ya wageni hatua iliyozua ghadhabu kote duniani.  Amri ya Trump: Ni nani anaathirika? Sudan yapinga amri ya Trump Amri ya Trump: Ni nani anaathirika? Waziri Mkuu Teresa May alitangaza muwaliko huo wakati akiwa ziarani Marekani. Afisi yake imesema japo haikubaliani na baadhi ya sera za Trump hata hivyo ni vyema Uingereza kuwa na ushirikiano wa karibu na Marekani. Kiongozi wa Upinzani Jeremy Corbyin ametaka Waziri Mkuu kuahiri