MAJALIWA KUHAMIA DODOMA LEO

Image result for kasimu majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuhamia rasmi leo mjini hapa ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa Julai 25, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mashujaa.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma imeandaa mapokezi ya Waziri Mkuu atakapowasili mchana na kuanzia kesho atafanya ziara ya siku mbili katika manispaa ya Dodoma kukagua hatua za maandalizi ya kupokea ujio wa Serikali.

Taarifa ya ofisi ya mkoa imesema Majaliwa atatembelea maeneo ya kutolea huduma za afya, kituo cha umeme cha Zuzu, masoko, chanzo cha maji cha Mzakwe na maeneo ya viwanda.

Ofisa habari wa mkoa, Jeremiah Mwakyoma amesema maandalizi yote muhimu kwa ajili ya mapokezi hayo yamekamilika.

Comments

Popular posts from this blog

ZINGATIA HAYA UKITAKA KURUDIANA NA MPENZI WAKO WA ZAMANI

ALAMA YA NYOKA KWENYE NEMBO MBALIMBALI INA MAANA KUBWA

Waziri Mkuu Ashangazwa Na Kodi Kubwa Soko La Dodoma.....Aagiza Baraza La Madiwani Lipitie Upya Na Kumpa Majibu