Posts

Wabunge Saba Wafukuzwa Bungeni Kwa Vitendo vya Vurugu Bungeni,Yumo Zitto,Mdee,Bulaya,Lissu....

Image
  Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge limepitisha azimio la kuwasimamisha kuhudhuria vikao vya Bunge baadhi ya wabunge wa Kambi ya Upinzani waliohusika katika kufanya vitendo vya vurugu ndani ya ukumbi na kudharau Mamlaka ya Spika Januari, 27, 2016.  Wabunge waliosimamishwa kuhudhuria vikao hivyo ni Mhe.Kabwe Zubeiri Ruyangwa Kabwe, Mhe.John Heche, Mhe.Halima Mdee,Mhe.Tundu Lissu, Mhe.Halima Mdee, Mhe.Pauline Gekul na Mhe. Ester Bulaya.  Azimio la adhabu kwa wabunge hao limetolewa na Bunge chini ya Kifungu cha 30A (1) cha sheria ya Haki Kinga na Madaraka ya Bunge Sura ya 296 na kanuni ya 74 (4) na (6).  Akisoma adhabu hizo Mwenyekiti wa kamati hiyo yenye wajumbe 15 Mhe.George Huruma Mkuchika amesema kuwa uchunguzi uliofanywa na Kamati hiyo kwa kuwaita na kuwahoji wahusika ulibaini kuwa wabunge hao walitenda kosa kwa kukiuka kanuni zinazoliongoza bunge hilo.  Imebainishwa kuwa Mhe.Zitto Kabwe alivunja mash...

MAANDALIZI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI TANZANIA 2016/2017 YAANZA RASMI

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dkt. Albina Chuwa akihojiwa na waandishi wa habari katika mkutano wa wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016. Mwenyekiti wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dkt. Fatuma Mrisho akielezea umuhimu wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 katika mkutano wa wadau wa utafiti huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016. Mkurugenzi Mkazi wa ICAP Tanzania Dkt. Fernando Morales akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa mwaka 2016/2017 uliofanyika jana jijini Dar es Salaam. Utafiti huo utafanyika nchi nzima kuanzia mwezi Agosti, 2016. (P.T) Baadhi ya washiriki waliohudhuria Mkutano wa Wadau wa Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI Tanzania wa...

Mbunge Amtaja Kikwete Sakata la EPA

Image
Mbunge wa Konde Khatibu Said Haji (Cuf), jana aliibua sakata la Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) bungeni akimtaja Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete kwamba alikiuka Katiba kwa kutoa msamaha kwa watu waliotuhumiwa. Hata hivyo, Serikali kupitia kwa Waziri wa Katiba na Sheria Dk Harrion Mwakyembe ilikanusha madai hayo na kusema Rais alikuwa sahihi kwa kuwa viko vifungu ambavyo vinampa nafasi hiyo. Katika swali la nyongeza, mbunge huyo alihoji ni kwa nini Kikwete alitoa msamaha kwa watu hao kabla hawajahukumiwa na Mahakama kama Katiba inavyosema.  “Kama hivyo ndivyo, basi naomba ukubali kuwa Kikwete (Rais mstaafu) alivunja Katiba ya nchi kwa kuwapa msamaha watuhumiwa wa EPA ambao walikuwa hawajahukumiwa bado, naomba majibu,”  alihoji Haji. Katika swali la msingi Mbunge huyo alitaka kujua iwapo Rais kwa mujibu wa Ibara ya 45 (1) A hadi D anayo mamlaka ya kutoa msamaha kwa watuhumiwa wa uhalifu wa aina yoyote ambao mashauri yake yapo katika vyombo vya dola kwenye ...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumanne ya May 31

Image

Wahitimu Sita wa Mafunzo ya JKT Wafikishwa Mahakamani Sakata la Kudai Ajira

Image
  WAHITIMU sita wa mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka matatu ikiwemo kufanya mkusanyiko usio halali na kushawishi wenzao kuandamana kwenda Ikulu kudai ajira, anaandika Faki Sosi.  Washtakiwa katika kesi hiyo ni George Mgoba, mwenyekiti wao; Parali Kiwango, makamu mwenyekiti; Linus Steven, katibu wa umoja wa wahitimu hao na wahitimu wengine, Emmanuel Mwasyembe, Ridhiwani Ngowi na Jacob Mang’wita.  Akiwasomea mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi, Respicius Mwijage, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Benard Kongola amesema, washitakiwa hao wanadaiwa kwamba 15 Februari 2014 katika eneo la Msimbazi Centre, Ilala Dar es Salaam walipanga njama za kutenda makosa hayo.  Katika shitaka lingine watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali kwa lengo la kuandamana kwenda kwa Rais kulazimisha kupewa ajira katika utumishi wa umma, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na kwamba, hatua hiyo ingesab...

UONGOZI WA UDSM WAANZA KUWEKA TAA MABIBO HOSTELI

Image
UONGOZI Chuo Kikuu cha Dar es salam unatarajia kununua taa za dharura 12 kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la giza katika Hosteli ya Mabibo. Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Naibu Makamu mkuu wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) anaeshughulikia masuala ya Utawala Prof.David Alfred Mfinanga wakati wa mahojiano na Idara ya Habari. Alisema kuwa tatizo la giza nene katika eneo hilo la lango kuu la kuingia Hostel za mabibo mpaka eneo lile la maegesho ya magari lipo mbioni kupatiwa ufumbuzi baada ya taratibu za ununuzi kukamilika. Alisema kuwa kukamilika kwa uwekaji wa taa hizo za dharura zitapunguza kabisa tatizo hilo. Aidha, Prof.David Alfred Mfinanga alisema kuwa katika mpango wa muda mrefu wa kutatua tatizo hizo uongozi wa UDSM unatarajia kuweka umeme wa jua ambao utapunguza gharama za kulipia umeme na hivyo kuwa na umeme wa uhakika. Hostel hizo za kisasa zilizojengwa miaka michache iliyopita na Shirika la Hifadhi za Jamii(NSSF) zimesaidia kupunguza tatizo...

Baada ya Kusimamishwa Kuhudhuria Vikao vya Bunge, Zitto Kabwe Acharuka

Image
Rais Magufuli tunakuunga mkono kwa dhati kupambana dhidi ya ufisadi. Tunakupinga kwa nguvu zote kupambana dhidi ya demokrasia. Kuanzia mwanzo tumekuunga mkono dhidi ya ukwepaji kodi, ubadhirifu, uvivu na uzembe. Tangia mwanzo tulionya kuwa ni lazima udhibitiwe na Bunge ili ufanye kazi kwa mujibu wa Katiba. Hivi sasa wewe Rais ndio unaendesha Bunge kwa remote control. Tutakupinga kuturudisha nyuma. Hutafanikiwa kamwe kubomoa misingi ya taasisi za uwajibikaji tulizoanza kuzijenga. Narudia nukuu muhimu sana " ukitaka kutawala tawala peke yako. Ukitaka kuongoza ongoza na wenzako". Rais Magufuli Tanzania inataka uongozi madhubuti na sio itawapendeza wa imla. Huko tumeshatoka na Watanzania hawatakubali kurudi huko. Haya kayaandika kwenye ukurasa wake wa Facebook